Tuesday, March 18, 2014



SIRI za kushindwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kwenye chaguzi mbalimbali yabainika,na kama chama hicho isipotafuta ufumbuzi wa siri hiyo basi kisubili miujiza kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Huku ikiwa ni siku moja imepita Baada ya Kumalizika Uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Kalenga na Chama cha Mapinduzi CCM kuibuka mshindi na kuigalagaza vibaya sana Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,
Uchunguzi uliofanywa na Mwandishi wa Mtandao huu umebaini udhaifu wa Kusimamia misimamo yao wanayoitoa kwa viongozi wa Juu wa chama hicho akiwemo Mwenyekiti wake Freeman Mbowe na Katibu Dokta Slaa ni miongoni za sababu chama hicho kufanya vibaya na kuendelea kufanya Vibaya kwenye chaguzi mbalimbali zinazokuja ikiwemo wa Serikali za Mitaa.

Sababu kubwa iliyogundulika inakitafuana chama hicho ni Idadi ndogo ya Vijana wenye umri wa miaka 18 ambao ni hazina kubwa ya Chama hicho kutoandikishwa kwenye Daftari la kupiga kura na hata wale walioandikisha nao wamepoteza Shahada za kupiga kura.
Duru hizo zinasema kwa mujibu wa tafiti mbalimbali zinaonyesha vijana Takribani Milioni kumi waliofikisha umri wa kupiga kura kisheria hawajaandikishwa kwenye Daftari hilo huku wengine waliojiandikisha teyari wamekufa huku taarifa zao hazijafika katika Tume hiyo ya uchaguzi.
Kwa Mujibu wa tume ya Uchaguzi nchini wamesema wao hawana Fedha za kuboresha Daftari hilo,huku ikumbukwe mara ya mwisho Daftari lilifanyiwa marekebisho mwaka 2009 na mpaka sasa miaka mitano imepita huku bado alijafanyiwa marekebisho.

Kile kinachotafsriwa na wengi uwenda uwezo mdogo wa viongozi hao Juu wa Chama hicho, katika kusimamia misimamo wanayoyasema,ama viongozi hao wanakuwa wanataka umaharufu wakisiasa kwa wanachama wao.
Ikumbukwe Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe katika mkutano wake na waandishi wa Habari uliofanyika miezi miwili iliyopita aliutangazi Umma wa Tanzania Chama hicho hakitashiriki Uchaguzi wowote Mpaka Daftari la kudumu la kupiga kura litakapoboreshwa.

Mbowe, ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Hai na vilevile kiongozi wa Kambi ya upinzani Bungeni alizidi kusema wao chadema wamebaini Vijana zaidi ya milioni Nane hawana kadi za kupigia huku tayari wamefikisha umri wa miaka 18 na wengine wamepoteza kadi zao na kuipa onyo kali tume ya Uchaguzu nchini kuboresha Daftali lasivyo chama hicho akitashiriki chaguzi zozote za nchi hii.
Lakini viongozi hao kuonyesha ugeugeu kwa wanachama wao katika kusimamia misimamo wanayoitoa , Hivi leo Chama hicho Kiendelea kushiriki kwenye Chaguzi mbalimbali hapa nchini huku kikijua kabisa hazina yao kubwa ni vijana ambao hawana Kadi za kupigia kura na huku chama cha Mapinduzi CCM kikitumia nguvu kubwa ya Wanachamma wazee hukuwakijua wanachama wengi wa Chadema ni Vijana kutilia fitina kwenye Tume ya Uchaguzi nchini.

Chadema ambacho ndicho chama Kikuu cha upinzani Nchini,ni Dhahiri viongozi wake ni wababaishaji kwa wananchama wake ndio maana wanashindwa kusimamia matamshi wanayoyatoa,
Swali la kujiuliza Viongozi wa Chadema mpaka wanaingia kwenye uchaguzi wa Kalenga walikuwa hawafahamu kuhusu hoja ya Daftari la kupiga kura? Je iko wapi misimamo ya Mwenyekiti wa Chadema kwamba watasusia Uchaguzi mpaka Daftali la wapiga kura litakapoboreshwa?

Mbowe na Katibu wake Dokta Slaa walikuwa wanawadanganya Wananchi au tuanze kutilia Shaka viongozi hao walipewa kitu kidogo na Tume ya Uchaguzi mpaka wakaingia kwenye uchaguzi wa Kalenga?
Na leo hii Tayari Chama hicho kimethibitisha Kushiriki kwenye Uchaguzi wa Jimbo la Chalinze Je kunahaja Gani chama hicho kushiriki kwenye uchaguzi huo huku kikijua hakina wanachama wakuweza kuwasaidia kushinda uchaguzi huo?

Au, Dhana ijengeke viongozi Hao wanapenda kuteketeza pesa kwenye Kampeni kwa kutumia Chopa angani huku wakijua kabisa hawana wanachama wakuwapa Dola,Chadema kina viongozi wakutoa matamko na kuwa na nyuso za kujiamini kutoa matamko pasipo kusimamia misimamo yao.

Tukitoa uchaguzi wa Chalinze kunaujaguzi wa Serikali za mitaa Je kwa mfumo huu wa Daftali la wapiga kura kutoboreshwa na kuwapa Fursa wananchi kusajiliwa je chama hicho kitegemee kushinda kwenye uchaguzi huo.
Kwa Tafsiri hii Uchaguzi wa Mdogo wa madiwani pamoja na Jimbo la Kalenga ingekuwa Ndoto kwa chama hicho kushinda kutokana na idadi ndogo ya wanachama.

Wanachama wa Chadema wanahaja ya kuwaangaliwa Viongozi wao wa Juu kwa makini sana wasiwabeze watu wanaowapinga viongozi hao wa juu kwakuwa wanahoja ya kuwapinga kwakuwa wamekuwa ni watu wa porojo tuu na sasa wananchi wameanza kuzichoka porojo zao na kuanza kuwasulubu kwenye chaguzi mbalimbali.

0 comments:

Post a Comment