Thursday, March 13, 2014



Habari zilizopatikana mchana huu kutoka visiwani Zanzibar zinasema kuwa vijana wenye mikokoteni inayovutwa na Ng'ombe wamefanya vurugu na kuanza kupiga mawe magari ya serikali huku wakijerui wafanyakazi wa serikali kadhaa. Katika kadhia hiyo, walisababisha gari la Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Uchumi,  Mhe. Khamis Musa kupinduka kama linavyoonekana pichani. Inaelezwa kuwa chanzo cha vurugu hizo ni kupigwa marufuku kwa mikokoteni hiyo kuingia mjini, kitendo ambacho kinapingwa na wamiliki.

0 comments:

Post a Comment