Saturday, March 22, 2014

Picha iliyotolewa na vyombo vya habari vya China vikionyesha kitu kipya kilichogunduliwa na satellite za nchi hiyo kikielea katika Bahari ya Hindi ambacho kinahisiwa huenda kikawa na uhusiano na ndege ya Malaysia iliyopotea.
Picha za Satellite kutoka kituo cha utafiti cha Marekani kikionyesha eneo ambako msako mkali unaendelea kuitafuta ndege iliyopotea huko katika bahari ya Hindi.
Hussein aliwaambia waandishi wa habari jijini Kuala Lumpur: 'Balozi wa China amepokea picha ya kitu kinachoelea kusini mwa bahari ya Hindi na amesema watatuma meli kuchunguza.
Muakilishi wa Waziri Mkuu wa Australia Warren akiongea na waandishi wa habari RAAF Pearce Base.
Ofisa wa anga, Peter Moore, ambaye pia ni rubani, amesema mchanganyiko wa hali ya hewa nchi kavu na ile ya bahari unaathiri ndege za uokoaji.
•    Waziri wa Mawasiliano Malaysia atangaza picha mpya ya Satellite
•    Asema China imetuma meli kuchunguza
•    Ni wiki mbili sasa tokea ndege hiyo ipotee
Kipande kikubwa cha chuma kimeonekana kikielea katika bahatri ya Hindi. Picha za Satellite za China zimeona  kipande chenye urefu wa futi 72 kiasi cha maili 75 mashariki mwa Australia.
Picha hizo zimechukuliwa siku mbili tu baada ya mamlaka za Australia kuona kitu kinachoelea katika pwani ya bahari ya Hindi.
CHANZO NI DAILY MAILY.

0 comments:

Post a Comment